Mpumbavu hataitwa tena mwungwana, wala ayari hatasemwa kwamba ni karimu.
Bali mwungwana huwaza mambo ya kiungwana, naye hushika sana mambo ya kiungwana.
Kwa maana imeandikwa ya kuwa, Ibrahimu alikuwa na wana wawili mmoja kwa mjakazi, na mmoja kwa mwungwana.
Lakini yule wa mjakazi alizaliwa kwa mwili, yule wa mwungwana kwa ahadi.
Bali Yerusalemu wa juu ni mwungwana, naye ndiye mama yetu sisi.
Lakini lasemaje andiko? Mfukuze mjakazi na mwanawe, kwa maana mwana wa mjakazi hatarithi kabisa pamoja na mwana wa mwungwana.
Ndiposa, ndugu zangu, sisi si watoto wa mjakazi, bali tu watoto wa huyo aliye mwungwana.
Hapo hapana Myunani wala Myahudi, kutahiriwa wala kutokutahiriwa, mgeni wala mshenzi, mtumwa wala mwungwana, bali Kristo ni yote, na katika yote.
Na wafalme wa dunia, na wakuu, na majemadari, na matajiri, na wenye nguvu, na kila mtumwa, na mwungwana, wakajificha katika pango na chini ya miamba ya milima,