Skip to Content

"shuhuda"

30 mara katika SUV

uyashike mausia ya Bwana, Mungu wako, uende katika njia zake, uzishike sheria zake, na amri zake, na hukumu zake, na shuhuda zake, sawasawa na ilivyoandikwa katika torati ya Musa, upate kufanikiwa katika kila ufanyalo, na kila utazamako;

Wakazikataa sheria zake, na agano lake, alilolifanya na baba zao; na shuhuda zake alizowashuhudia; wakafuata ubatili, wakawa ubatili, nao wakaandamana na mataifa waliowazunguka, ambao Bwana alikuwa amewaagiza, wasitende kwa mfano wao.

Mfalme akasimama karibu na nguzo, akafanya agano mbele za Bwana, kumfuata Bwana, na kuyashika maagizo yake, na shuhuda zake, na amri zake, kwa moyo wake wote, na kwa roho yake yote, na kuyathibitisha maneno ya agano hilo yaliyoandikwa katika kitabu hicho; nao watu wote wakalikubali agano lile.

Njia zote za Bwana ni fadhili na kweli, Kwao walishikao agano lake na shuhuda zake.

Lakini walimjaribu Mungu Aliye juu, wakamwasi, Wala hawakuzishika shuhuda zake.

Katika nguzo ya wingu alikuwa akisema nao. Walishika shuhuda zake na amri aliyowapa.

Heri wazitiio shuhuda zake, Wamtafutao kwa moyo wote.

Nimeifurahia njia ya shuhuda zako Kana kwamba ni mali mengi.

Uniondolee laumu na dharau, Kwa maana nimezishika shuhuda zako.

Shuhuda zako nazo ndizo furaha yangu, Na washauri wangu.

Nimeambatana na shuhuda zako, Ee Bwana, usiniaibishe.

Unielekeze moyo wangu na shuhuda zako, Wala usiielekee tamaa.

Nitazinena shuhuda zako mbele ya wafalme, Wala sitaona aibu.

Nalizitafakari njia zangu, Na miguu yangu nalizielekezea shuhuda zako.

Wakuchao na wanirudie, Nao watazijua shuhuda zako.

Unihuishe kwa fadhili zako, Nami nitazishika shuhuda za kinywa chako.

Wasio haki wameniotea ili kunipoteza, Nitazitafakari shuhuda zako.

Ninazo akili kuliko wakufunzi wangu wote, Maana shuhuda zako ndizo nizifikirizo.

Shuhuda zako nimezifanya urithi wa milele, Maana ndizo changamko la moyo wangu.

Wabaya wa nchi pia umewaondoa kama takataka, Ndiyo maana nimezipenda shuhuda zako.

Mimi ni mtumishi wako, unifahamishe, Nipate kuzijua shuhuda zako.

Shuhuda zako ni za ajabu, Ndiyo maana roho yangu imezishika.

Umeziagiza shuhuda zako kwa haki, Na kwa uaminifu mwingi.

Haki ya shuhuda zako ni ya milele, Unifahamishe, nami nitaishi.

Nimekuita Wewe, uniokoe, Nami nitazishika shuhuda zako.

Tokea zamani nimejua kwa shuhuda zako, Ya kuwa umeziweka zikae milele.

Wanaonifuatia na watesi wangu ni wengi, Lakini sikujiepusha na shuhuda zako.

Nafsi yangu imezishika shuhuda zako, Nami nazipenda mno.

Nimeyashika mausia yako na shuhuda zako, Maana njia zangu zote zi mbele zako.

Wanao wakiyashika maagano yangu, Na shuhuda nitakazowafundisha; Watoto wao nao wataketi Katika kiti chako cha enzi milele.