Ingawa uovu una tamu kinywani mwake, Ingawa auficha chini ya ulimi wake;
Tumbo lililomzaa litamsahau; buu litamla na kuona tamu; Hatakumbukwa tena; Na udhalimu utavunjwa kama mti.
Tulipeana shauri tamu; na kutembea Nyumbani mwa Mungu pamoja na mkutano.
Maneno yapendezayo ni kama sega la asali; Ni tamu nafsini, na afya mifupani.
Mwanangu, ule asali, kwa maana ni njema, Na sega la asali lililo tamu ulionjapo.
Basi utaijua hekima kuwa tamu kwa nafsi yako; Ikiwa umekwisha kuiona; Ndipo itakapofuata thawabu; Wala tumaini lako halitabatilika.
Kweli nuru ni tamu, tena ni jambo la kupendeza macho kutazama jua.
Hua wangu, mafichoni mwa jabali, Katika sitara za magenge, Nitazame uso wako, nisikie sauti yako, Maana sauti yako ni tamu na uso wako mzuri.
Akaniambia, Mwanadamu, lisha tumbo lako, ulijaze tumbo lako kwa hili gombo nikupalo. Ndipo nikalila, nalo kinywani mwangu lilikuwa tamu, kama utamu wa asali.
Angalieni, siku zinakuja, asema Bwana, ambazo huyo alimaye atamfikilia avunaye, na yeye akanyagaye zabibu atamfikilia apandaye mbegu; nayo milima itadondoza divai tamu, na vilima vyote vitayeyuka.