Maana fadhili zako zi mbele ya macho yangu, Nami nimekwenda katika kweli yako.
Nitamhimidi Bwana kila wakati, Sifa zake zi kinywani mwangu daima.
Ee Mungu, nadhiri zako zi juu yangu; Nitakutolea dhabihu za kushukuru.
Mhesabieni Mungu nguvu; Enzi yake i juu ya Israeli; Na nguvu zake zi mawinguni.
Bwana, zi wapi fadhili zako za kwanza, Ulizomwapia Daudi kwa uaminifu wako?
Siku zangu zi kama kivuli kilichotandaa, Nami ninanyauka kama majani.
Mwanadamu siku zake zi kama majani; Kama ua la kondeni ndivyo asitawivyo.
Nimeyashika mausia yako na shuhuda zako, Maana njia zangu zote zi mbele zako.
Kwa maana njia za mwanadamu zi mbele za macho ya Bwana, Na mienendo yake yote huitafakari.
Dhambi za watu wengine zi dhahiri, zatangulia kwenda hukumuni; wengine dhambi zao zawafuata.