Zaburi Chapter 137
1
Kando ya mito ya Babeli ndiko tulikoketi, Tukalia tulipoikumbuka Sayuni.
2
Katika miti iliyo katikati yake Tulivitundika vinubi vyetu.
3
Maana huko waliotuchukua mateka Walitaka tuwaimbie; Na waliotuonea walitaka furaha; Tuimbieni baadhi ya nyimbo za Sayuni.
4
Tuuimbeje wimbo wa Bwana Katika nchi ya ugeni?
5
Ee Yerusalemu, nikikusahau wewe, Mkono wangu wa kuume na usahau.
6
Ulimi wangu na ugandamane Na kaakaa la kinywa changu, nisipokukumbuka. Nisipoikuza Yerusalemu Zaidi ya furaha yangu iliyo kuu.
7
Ee Bwana, uwakumbuke wana wa Edomu, Siku ya Yerusalemu. Waliosema, Bomoeni! Bomoeni hata misingini!
8
Ee binti Babeli, uliye karibu na kuangamia, Heri atakayekupatiliza, ulivyotupatiliza sisi.
9
Heri yeye atakayewakamata wadogo wako, Na kuwaseta wao juu ya mwamba.