Zaburi Sura 121
1
Nitayainua macho yangu niitazame milima, Msaada wangu utatoka wapi?
2
Msaada wangu u katika Bwana, Aliyezifanya mbingu na nchi.
3
Asiuache mguu wako usogezwe; Asisinzie akulindaye;
4
Naam, hatasinzia wala hatalala usingizi, Yeye aliye mlinzi wa Israeli.
5
Bwana ndiye mlinzi wako; Bwana ni uvuli mkono wako wa kuume.
6
Jua halitakupiga mchana, Wala mwezi wakati wa usiku.
7
Bwana atakulinda na mabaya yote, Atakulinda nafsi yako.
8
Bwana atakulinda utokapo na uingiapo, Tangu sasa na hata milele.